Monday, July 26, 2010
Sunday, July 25, 2010
WAGOMBEA UDIWANI VITI MAALUMU ARUMERU WAPINGA MATOKEO
Richard Mwangulube Arusha
Wagombea Udiwani wa UWT kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Arumeru wamepiga matokeo yaliyotangzwa jana wakati wa Uchaguzi wa Jumuiya hiyo ya Chama kwa madai kuwa Uchaguzi huo ulitawaliwa na mizengwe pamoja na ubabe.
Wagombea hao pamoja na baadhi ya Wanachama wa Jumuiya hiyo ya wapatao 23 tayari wamewasilisha rufaa yao kwa katibu wa CCM wa mkoa wa Arusha na nakala kupelekwa kwa Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Taifa, Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Mkoa wa Arusha pamoja na Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa nchini(TAKUKURU) .
Katika kupinga matokeo hayo wamesema uchaguzi huo uliendeshwa bila kuzingatia kanuni , taratibu na sheria zinazoongoza shughuli za uchaguzi ndani ya jumuiya hiyo ama Chama cha Mapinduzi.
Aidha Walalamikaji hao wamesisitiza kuwa matokeo ya uchaguzi huo ulikuwa na mwelekeo mzima wa kuwepo na upangaji wa matokeo kutokana na kuendeshwa kwa ubabe.
Wamesema wakati wa kuhesabu kura wagombea walikataliwa kutuma wawakilishi wao kwa ajili ya kushuhudia kura zao pia baadhi ya watendaji wa UWT wilaya akiwemo katibu wa UWT Wilaya waliendelea kusimamia shughuli za uchaguzi licha ya watendaji hao kuwa wagombea.
Msimamizi wa uchaguzi alitoa matokeo tofauti na yalivyokuwa na kusababisha mshangao katika ukumbi huo kutokana na kubabaika na hivyo wametaka uchaguzi huo kurudiwa tena ama kura kuhesabiwa upya.
Katibu wa UWT Wilaya Frida Kaaya alipotafutwa kwa njia ya simu hakuweza kupatikana kabisa wakati Katibu wa UWT Mkoa wa Arusha Elly Minja alipohojiwa kwa njia ya simu alisema hilo ni jukumu la Wilaya na sio la Mkoa.
mwisho
Wagombea Udiwani wa UWT kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Arumeru wamepiga matokeo yaliyotangzwa jana wakati wa Uchaguzi wa Jumuiya hiyo ya Chama kwa madai kuwa Uchaguzi huo ulitawaliwa na mizengwe pamoja na ubabe.
Wagombea hao pamoja na baadhi ya Wanachama wa Jumuiya hiyo ya wapatao 23 tayari wamewasilisha rufaa yao kwa katibu wa CCM wa mkoa wa Arusha na nakala kupelekwa kwa Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Taifa, Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Mkoa wa Arusha pamoja na Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa nchini(TAKUKURU) .
Katika kupinga matokeo hayo wamesema uchaguzi huo uliendeshwa bila kuzingatia kanuni , taratibu na sheria zinazoongoza shughuli za uchaguzi ndani ya jumuiya hiyo ama Chama cha Mapinduzi.
Aidha Walalamikaji hao wamesisitiza kuwa matokeo ya uchaguzi huo ulikuwa na mwelekeo mzima wa kuwepo na upangaji wa matokeo kutokana na kuendeshwa kwa ubabe.
Wamesema wakati wa kuhesabu kura wagombea walikataliwa kutuma wawakilishi wao kwa ajili ya kushuhudia kura zao pia baadhi ya watendaji wa UWT wilaya akiwemo katibu wa UWT Wilaya waliendelea kusimamia shughuli za uchaguzi licha ya watendaji hao kuwa wagombea.
Msimamizi wa uchaguzi alitoa matokeo tofauti na yalivyokuwa na kusababisha mshangao katika ukumbi huo kutokana na kubabaika na hivyo wametaka uchaguzi huo kurudiwa tena ama kura kuhesabiwa upya.
Katibu wa UWT Wilaya Frida Kaaya alipotafutwa kwa njia ya simu hakuweza kupatikana kabisa wakati Katibu wa UWT Mkoa wa Arusha Elly Minja alipohojiwa kwa njia ya simu alisema hilo ni jukumu la Wilaya na sio la Mkoa.
mwisho
WANAJESHI WALIOPIGANA VITA KUU WAILALAMIKIA SERIKALI
WAZEE WALIOPIGANA VITA YA PILI WALALAMIKA KUTORIDHIKA NA WALIVYOTENDEWA NA SERIKALI
Richard Mwangulube,Arusha
Wananchi wa Mkoa wa Arusha leo wameadhimisha siku ya mashujaa kwa kupambwa na gwaride la gadi moja ya jeshi la mgambo wakiongozwa na bendi ya Chuo cha jeshi nchini[TMA] kilichopo Monduli.
Maadhimisho hayo yamefanyika mbele ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwenye mnara wa kumbukumbu ya askari wa waliopigana katika vita vya Kagera.
Wakati wa maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa na Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa huo Jowika Kasunga (Monduli) , Raymond Mushi( Arusha)Mercy Silla( Arumeru) Elias Wawalali ( Ngorongoro) na James Ole Millya wa Longido pamoja na wakurugenzi wa halmashauri za wilaya na jiji la Arusha .
Sherehe hizo pia zimehudhuriwa na wakuu wa vikosi vya ulinzi na usalama mkoani hapa pamoja na Kamati za ulinzi na usalama, watendaji wakuu wa idara ya Serikali na taasisi za Umma.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Isidore Shirima aliweka ngao na mkuki, mshauri wa mgambo S.S. Mkumbo aliweka upinde, wakati askari wa mstaafu wa Jeshi la wananchi wa Tanzania(JWTZ),Kanali Mstaafu Gunzu aliweka shoka.
Askari aliyepigana vita kuu ya pili mwenye namba T 946 mzee Eliam Mrabundi aliweka sime katika mnara huo wakati Mkurugenzi wa Jiji Raphael Mbunda yeye aliweka Maua.
Hata hivyo akizungumz amara baada ya kuhitimishwa kwa shughuli hizo, mzee Eliam Mrabundi ambaye alipigana vita kuu ya pili ameelezea maskitiko yake na kudai kuwa pamoja na mchango wao huo lakini hadi leo hii hawajalipwa fedha zao tangu aliporejea Nchini kutoka Misri mara baada ya kumalizika kwa hiyo.
Aidha Mzee huyo ameelezea masikitiko yake hayo na kwamba hata baada ya uhuru Serikali imeshindwa kuthamini mchango wa wazee hao waliotetea nchi na baadhi yao kupoteza maisha yao
Nao askari wastaafu wa JWTZ wamesema pamoja na kushiriki katika harakati za kulinda nchi na kujitolea kwanda Msumbiji na kupigana katika vita vya Kagera lakini wengi wao hawajalipwa fedha zao hadi sasa.
Subscribe to:
Comments (Atom)